FAHAMU MADARAJA YA MOTO

 1.7 MADARAJA YA MOTO 

Kuna umuhimu mkubwa wa mtu yeyote kufahamu aina ya moto uliotokea ili aweze 

kuuzima kwa usalama na usahihi kwa kutumia kizimio sahihi ili kuepuka madhara 

yanayoweza kusababishwa na huo moto, ikiwa ni pamoja na kuendelea kuwaka au 

kusambaa kwenye sehemu zingine zilizo salama. 

Kuna madaraja manne ya moto ambayo ni kama ifuatavyo: 

DARAJA LA KWANZA 

Hili daraja linahusisha mioto yote yenye asili ya mimea kama vile makaratasi, nguo, 

mbao, kuni, majani, miti n.k. 

(Hapa kizimio sahihi ni maji) 

DARAJA LA PILI 

Hili daraja linahusisha mioto ya vimiminika vinavyolipuka na kuwaka kama vile 

petroli dizeli mafuta ya taa, rangi ya mafuta, mafuta ghafi, mafuta ya kupikia n.k. 

(Kizimio sahihi cha mioto ya vimiminika vinavyowaka ni fomu, unga mkavu, blanketi 

ya kuzimia moto, na mchanga mkavu) 

DARAJA LA TATU 

Daraja hili linahusisha mioto ya gesi kama vile gesi asilia na gesi za viwandani mfano 

Songas, Propen, Methen.pia daraja hili utapata mioto inayotokana na kifaa 

kinachotumia umeme kuungua.Ikumbukwe kuwa hakuna moto wa umeme ila 

umeme ni chanzo kikubwa cha moto. 

(Kizimio sahihi ni kufunga valve ya gesi inayotoka kwenye mtungi uliohifadhi gesi.) 

Kisha kutumia unga maalumu(DC au DP) 

DARAJA LA NNE 

DARAJA hili linahusisha mioto inayohusisha vyuma kama vile 

Aluminium,Zink,Kopa(copper) ,makaa ya mawe n.k 

(Kizimio sahihi ni ‘Unga maalumu.usitumie maji) 

Comments

Popular Posts